Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Wizara Ya Ardhi Na Maendeleo Ya Makaazi Zanzibar Imeshauriwa Kueka Mikakati Madhubuti Ya Kutoa Elimu Kwa Umma Kuhusu Uzingatiaji Wa Sheria Kanuni Na Taratibu Zinazohusiana Na Sekta Ya Ardhi

Mhe Yahya Rashid Abdallah akitoa ushauri baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya wizara hiyo kwa kipindi cha april hadi Juni 2021 – 2022.

 Wajumbe wa kamati ya mawasiliano ardhi na  nishati ya Baraza la Wawakilishi chini ya Mwenyekiti wake Mhe Yahya Rashid Abdallah wametoa ushauri huo baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya wizara hiyo kwa kipindi cha april hadi Juni 2021 – 2022.

Wamesema dhamira ya serikali ni kuifanya ardhi kuwa kichocheo cha maendeleo na nyenzo muhimu katika kupambana na umaskini.

Katibu Mkuu  Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi dkt Mngereza Mzee Miraj akiwasilisha utekelezaji wa wizara  hio ameieleza kamati kwamba wizara inaendelea na utaratibu wa uaandaaji wa rasimu ya sera ya mipango miji na vijiji ili kuhakikisha uwepo wa miji na vijiji bora na vya kisasa.