




Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi
Napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha kwa dhati katika tovuti rasmi ya Wizara ya Maendeleo ya Ardhi na Makazi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kupitia tovuti hii, tumedhamiria kutoa taarifa sahihi, za uhakika na kwa wakati kuhusu shughuli mbalimbali tunazozitekeleza katika kusimamia na kuendeleza sekta muhimu ya ardhi na makazi kwa maendeleo ya jamii yetu.
Wizara hii imeanzishwa kwa Tangazo la Kisheria Na. 137 la mwaka 2020 na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa chini ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 (Toleo la 2010), ikiwa na jukumu kubwa la kuhakikisha usimamizi bora wa ardhi, upangaji miji, usajili wa ardhi, umilikishaji, na ujenzi wa makazi ya kisasa na nafuu kwa wananchi wa Zanzibar.
Kwa kuzingatia historia ya sekta hii tangu Mapinduzi ya mwaka 1964, Wizara yetu imepitia hatua mbalimbali za mabadiliko ya kimfumo, hadi kufikia sura yake ya sasa kama taasisi madhubuti inayolenga kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuzingatia weledi, uwazi, na ufanisi. soma zaidi ……….
Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar
Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi
N/Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi
N/Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi

