DK. MNGEREZA: SMZ IMEFUNGUA MILANGO YAKE KWA KUWAKARIBISHA WAWEKEZAJI KUJA KUEKEZA ZANZIBAR
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeweka mazingira rafiki kwa kuzifanyia marekebisho sheria zake ili kutoa fursa kwa wawekezaji kuja kuekeza Zanzibar. Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Dkt. Mngereza Mzee Miraji ameeleza hayo katika mazungumzo maalum yaliowashirikisha ujumbe kutoka European Mortgage Federation na taasisi inayoshughulikia masuala ya mikopo ya ujenzi wa nyumba ya […]