Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Mkurugenzi Ldara Ya Utumishi Na Uendeshaji Kutoka Wizara Ya Ardhi Na Maendeleo Ya Makaazi Bi.Khamisuu Hamid Mohammed Amesema Mfumo Wa Manunuzi Kwa Njia Ya Kimtandao Utawezesha Taasisi Kufanyakazi Kwa Ufanisi Na Kuondokana Na Udanganyifu.


Akizungumza wakati alipokua  akifungua  mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyakazi wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kupitia mfumo mpya wa manunuzi kimtandao Mkurugenzi Hamisuu aliwataka wafanyakazi hao kuyatumia ipasavyo mafunzo hayo ili kuweza kufikia lengo lililokusudiwa.

Alifahamisha kua mfumo huo ambao ulizinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwentekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi tarehe 25 july 2022 kwa lengo la kuhakikisha tunaondokana na kufanya manunuzi kwa njia ya kawaida na badala yake kuingia katika mfumo wa kisasa ili kuendana hali halisi ya sayansi na tecknolojia.

Akiwasilisha mada kuhusiana  na namna ya kuweza kuutumia mfumo huo muwezeshaji kutoka mamlaka ya ununuzi na uondoshaji Mali za umma Hafidh Rashid Zam amesema kua mfumo huo utaondosha ubinafsi katika masuala ya manunuzi kwani tayari umeshaungwa moja kwa moja kupitia  wakala  serikali mtandao e government na utakua unaonesha kazi zote za manunuzi zinazofanywa katika Taasisi.