Ameyasema hayo huko Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja katika ziara zake za ufatiliaji wa Migogoro ya Ardhi ilioko Paje na Kizimkazi inayohusisha uvamizi wa maeneo kinyume na utaratibu wa makubaliano ya wahusika.
Aidha amesema kuwa Wizara kupitia Kamati ya Usuluhishi na utatuzi wa Migogoro ya Ardhi mara baada ya kupokea malalamiko ya Wananchi yanayohusiana na Migogoro ya Ardhi baina yao hufanya jitihada za kufika maeneo husika ili kuweza kuthibitisha juu ya kilichowasilishwa na baadae kutolea maamuzi.