SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

WIZARA YA ARDHI NA MAEDELEO YA MAKAAZI

Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe Rahma Kassim Ali amewataka wafanayakazi wa ofisi ya mthamini mkuu wa serikali kuwa makini wakati wanapokagua ripoti za uthamini ili kuepuka udanganyifu katika kazi hiyo.

Aliyasema hayo katika ofisi za Taasisi hiyo Michenzani Mall katika kikao maalum kilichowashirikisha watendaji hao chenye lengo la kukuza ufanisi wa kiutendaji wa ofisi hiyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe Salha Mohammed Mwinjuma amesisitiza haja kwa watendaji hao kua na utaratibu wa kufanya ziara za kutembelea maeneo ambayo yanafanyiwa uthamini na ili kuweza kujirizisha mara baada ya kupokea ripotia za uthamini wa eneo husika

Mapema Mthamini Mkuu wa Serikali Tahir Mussa omar amefahamisha kuwa kwa Sasa Taasisi hiyo imefanikiwa kutayarisha muongozo wa Mali na malipo ya fidia kwa wafanyakazi ambao kwa sasa umeshaanza kufanyakazi.