Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi imeshauriwa kuhakikisha inaendelea na hatua ya utoaji wa Elimu kwa wananchi kuhusiana utaratibu wa Tozo za Ardhi.

Akizungumza katika kikao Maalumu cha Kamati ya Kanuni na Sheria ndogo ndogo ya Baraza la Wawakilishi kilichowashirikisha Wajumbe wa Kamati hiyo watendaji wakuu wa Taasisi pamoja na Wadau wa Kanuni huko katika Ukumbi wa Wizara ya Ardhi Ofisi kuu Pemba Mwenyekiti wa Kamati Mhe.Mihayo Juma Nunga amesema hatua hiyo itasaidia kuondoa Migongano katika Jamii.

Wakichangia mada kuhusiana na Gharama za Tozo hizo wajumbe hao wameiomba Wizara kuangalia uwezekano wa kupunguza Gharama za ulipaji ili Wananchi kuweza kuzimudu.

Akitoa ufafanuzi katika kikao hicho kuhusiana na masuala balimbali ya kanuni za Tozo za Ardhi Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe Salha Mohammed Mwinjuma amefahamisha kuwa Lengo kuu la kuundwa kwa Kanuni hiyo ni kuondosha changamoto zote zinazotokana na Migogoro ya Ardhi